Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Karibu
Hii ni chombo ya kukusaidia kutafuta habari mu vichapo vya Mashahidi wa Yehova mu luga mbalimbali.
Kama unapenda kuchukua kichapo fulani, tafazali fungua jw.org.
  • Leo

Siku ya Pili, 15 Mwezi wa 7

Chunga kondoo wangu wadogo.​—Yoh. 21:16.

Mutume Petro aliambia hivi wazee wenzake “Muchunge kundi la Mungu.” (1 Pe. 5:1-4.) Kama uko muzee, tunajua kama unapenda ndugu na dada zako na unapenda kuwahangaikia. Lakini, wakati fulani unaweza kuona kama uko na mambo mingi ya kufanya ao unachoka sana na hautaweza kutimiza ile daraka. Unaweza kufanya nini? Ambia Yehova mahangaiko yako. Petro aliandika hivi: “Kama mutu yeyote anatumikia, afanye hivyo kama vile anategemea nguvu zenye Mungu anatoa.” (1 Pe. 4:11) Pengine ndugu na dada zako wako napambana na magumu yenye haiwezi kumalizika kabisa mu hii ulimwengu. Lakini kumbuka kama “muchungaji mukubwa,” Yesu Kristo, anaweza kuwasaidia zaidi kuliko weye. Anaweza kufanya vile leo na pia mu dunia mupya. Mungu haombe wazee mambo mingi; anawaomba tu wapende ndugu zao, wahangaikie ndugu zao, na wakuwe “mifano kwa kundi.” w23.09 29-30 fu. 13-14

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2025

Siku ya Tatu, 16 Mwezi wa 7

Yehova anajua kama kufikiri kwa watu wenye hekima ni kwa bure.​—1 Ko. 3:20.

Tunapaswa kuepuka kuwa na mawazo ya wanadamu wenye hawatii sheria za Yehova. Kama tunakuwa na mawazo sawa ya watu wenye hawamutii Yehova, siye pia tunaweza kumuacha Yehova na kuacha kutii sheria zake. (1 Ko. 3:19) Mara mingi “hekima ya ulimwengu huu” inachocheaka watu wasimutii Mungu. Wakristo fulani wa Pergamamu na Tiatira walichochewa na watu wenye waliishi nao wenye walikuwa waasherati na waabudu sanamu. Juu wale Wakristo waliachilia uasherati uendelee, Yesu aliwapatia mashauri mazito. (Ufu. 2:14, 20) Leo, watu wanaweza kufanya tukuwe na mawazo ya mubaya. Watu wa familia na marafiki wanaweza kutuambia kama tuko wenye kushikamana kupita kiasi na mambo yenye tunaamini na wanaweza kutuambia tuvunje sheria za Yehova. Kwa mufano, wanaweza kusema kama haiko jambo ya maana kuendelea kuwa na mwenedo safi na kama kanuni zenye kuwa mu Biblia kuhusu mwenendo ni mambo ya zamani. Wakati fulani tunaweza kuwaza kama maagizo yenye Yehova anatupatiaka haieleweke. Tunaweza hata kujaribiwa kuongeza mambo yenye “kupita mambo yenye yaliandikwa.”​—1 Ko. 4:6. w23.07 16 fu. 10-11

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2025

Siku ya Ine, 17 Mwezi wa 7

Rafiki wa kweli anapenda nyakati zote Naye ni ndugu mwenye amezaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu.​—Mez. 17:17.

Maria, mama ya Yesu, alikuwa na lazima ya kutiwa nguvu. Hakukuwa na bwana lakini alipaswa kupata mimba. Hakukuwa alishakomalisha mutoto yeyote, lakini sasa alipaswa kuhangaikia mutoto mwenye angefikia kuwa Masiya. Na juu alikuwaka hayafanya ngono, namna gani angefasiria Yosefu, muchumba wake, ile mambo yote? (Lu. 1:26-33) Maria alipata wapi nguvu? Alitafuta musaada kwa Yehova. Kwa mufano, alimuomba Gabrieli amupatie mafasirio zaidi kuhusu mugao wake. (Lu. 1:34) Kisha wakati kidogo alisafiri kuenda mu eneo ya “inchi ya milima” ya Yuda ili kutembelea Elizabeti, mutu wa jamaa yake. Elizabeti alimupongeza Maria na aliongozwa na Yehova ili kutoa unabii wenye kutia moyo kuhusu mwana wa Maria mwenye alikuwa hayazaliwa. (Lu. 1:39-45) Maria alisema kama Yehova alikuwa “ametenda kwa nguvu kwa mukono wake.” (Lu. 1:46-51) Yehova alimutia nguvu Maria kupitia Gabrieli na Elizabeti. w23.10 14-15 fu. 10-12

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hii ni chombo ya kukusaidia kutafuta habari mu vichapo vya Mashahidi wa Yehova mu luga mbalimbali.
Kama unapenda kuchukua kichapo fulani, tafazali fungua jw.org.
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine